Downloads

Entrance Form -F1 – 2025

Tafadhali pakua form hii na jaza taarifa sahihi katika fomu hii na rudisha ofisi ya usajili shule ya Sekondari Loyola Jengo la Utawala, chumba Na. A009. Mtihani wa kwanza wa Usahili (first interview) utafanyika siku ya Ijumaa, 20 Septemba 2024 saa 1:00 asubuhi na mwisho wa kurudisha Fomu ni siku ya Alhamisi, 19 Septemba 2024 saa Tisa Alasiri. Mtihani wa Pili wa Usahili (second interview) utafanyika siku ya Jumamosi, 28 Septemba 2024 saa 1:00 asubuhi na mwisho wa kurudisha Fomu ni siku ya Ijumaa, 27 Septemba 2024 saa Tisa Alasiri.
Mtihani wa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mkoani utafanyika siku ya Jumamosi, tarehe 28 Septemba 2024 saa mbili asubuhi. Mzazi/ mlezi unaombwa kurudisha fomu hii katika kituo atakachofanyia mtihani mwanafunzi. Vituo vya mtihani ni kama ifuatavyo:
 Mwanza – Mtihani wa usaili utafanyikia Parokia ya Nyakahoja na fomu zitarudishwa hapo hapo.
 Dodoma – Mtihani wa usaili utafanyikia Shule ya msingi ya Mt. Inyasi na fomu zitarudishwa hapo hapo
 Arusha na Moshi – Mtihani wa usaili utafanyikia Notre Dame shuleni Temdo, Njiro na fomu zitarudishwa hapo
hapo.
Mwanafunzi anapaswa kurudisha fomu hii ikiambatana na vitu vifuatavyo:

  1. (a) Nakala ya cheti cha kuzaliwa cha mwanafunzi au Hati ya kiapo cha mahakama inayothibitisha tarehe ya
    Kuzaliwa na jina kamili la mwanafunzi.
    (b) Mwanafunzi anapaswa kuwa amehitimu darasa la saba kabla ya 31 Disemba 2024. Mwanafunzi wa
    darasa la sita hastahili.
    (c) Picha mbili ndogo (Passport size) za mwanafunzi ambazo amepiga hivi karibuni.
    (d) Risiti ya malipo ya fomu. (fomu haitapokelewa bila risiti ya malipo)
  2. Sehemu ‘B’ ya fomu hii inapaswa kujazwa na Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi aliyosoma mwanafunzi.
  3. Gharama ya fomu ni Tshs. 25,000/=, mara baada ya kununua fomu pesa HAITARUDISHWA.